Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Serikali kuwalipa fidia wananchi wa Igunga waliopitiwa na bomba…

  • June 5, 2018June 5, 2018

Serikali imesema itahakikisha wananchi wa wilaya ya IGUNGA mkoani TABORA waliopitiwa na mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka HOIMA nchini UGANDA hadi mkoani TANGA wanalipwa fidia baada ya maeneo yao kufanyiwa tathmini.

Mkuu wa idara ya usafi na mazingira wilayani IGUNGA,FREDRICK MNAELA amesema wananchi waliopitiwa na mradi huo watalipwa fedha zao kwa wakati baada ya serikali kukamilisha tathmini ya maeneo husika.

Amesema wilaya ya IGUNGA ina kata ambazo zitanufaika na mradi  wa bomba la mafuta na kwamba baadhi ya kata itajengwa kambi ya mafundi wa ujenzi wa mradi huo.

Kwa upande wake,Afisa Mtendaji wa kijiji cha BULYANG’OMBE katika kata ya NANGA,SAID KIMENYA amesema anaamini kuwa wananchi waliopo katika kijiji chake watalipwa fidia zao huku akisema kambi ya bomba ya bomba la mafuta itajengwa kwenye kijiji hicho.

Naye mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha BULYANG’OMBE,ASHA RASHIDI amesema kwamba kupita kwa bomba la mafuta kutoka nchini UGANDA hadi bandari ya TANGA ni jambo zuri huku akisema wananchi wake watapata ajira.

Aidha mwananchi ambaye bomba lake litapitiwa na mradi huo katika eneo MIHAYO SHATILA amesema kuwa vitu mali zilizofanyiwa tathimni ni mazao amabyo yapo kwenye eneo lake.

Amesema kuwa anaamini serikali itatenda haki kwa wale wananchi ambao wanatakiwa kufidiwa ili waweze kutafuta maeneo mengine.

MWANDISHI:AVELIUS EVODIUS,CGFM.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Serikali wilayani TABORA itawachukulia hatua wananchi wanaochafua mazingira.
Serikali imetenga fedha kwa ajili ya Mfuko wa Watu wenye Ulemavu.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise