Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Burundi yapiga kura ya maoni kubadilisha katiba

  • May 17, 2018

Raia wa Burundi leo wanapiga kura ya maoni ya kubadilisha katiba, hatua ambayo itaweza kumpa Rais Piere Nkurunziza nafasi ya kuwa rais hadi mwaka 2034.

Wananchi wa Burundi wamejitokeza leo kushiriki mchakato wa kupiga kura ya maoni kuhusu mabadiliko ya katiba. Mabadiliko hayo ya katiba, yatakampa nafasi Rais Pierre Nkurunziza kuweza kutawala hadi 2034. Mchakato huo unafuatiliwa kwa karibu hasa na mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu. Hatua hiyo imezua hofu ya ukandamizaji mkubwa wa kisiasa na migogoro ya kikabila katika taifa hilo la Maziwa Makuu.

Karibu watu nusu milioni wamekimbia tokea Nkurunziza kushinda muhula wa tatu wa urais katika uchaguzi uliokuwa na ghasia wa mwaka 2015.

Nkurunziza, mwalimu wa zamani wa riadha na aliyekuwa kiongozi wa vita vya msituni kutoka katika kabila la wengi la Hutu, amekuwa akiliongoza taifa hilo tokea mwaka 2005 vilipomalizika vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyosababisha vifo vya watu 300,000.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Korea Kaskazini yafuta mkutano wa kilele na Korea Kusini
Watanzania wataka elimu iboreshwe- Utafiti.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise