Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Congo kuanzisha mfuko maalum kusimamia misaada ya kiutu

  • April 19, 2018April 19, 2018

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inapanga kuanzisha mfuko maalumu wa kusimamia misaada yote chini ya rasimu mpya ya sheria, wiki moja baada ya kushindwa kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa wafadhili mjini Geneva Uswisi. 

Ruanda Kiziba Flüchtlingslager (Reuters/J. Bizimana)

Umoja wa Mataifa unatafuta kiasi cha dola bilioni 2.2 ili kuwasadia watu milioni 13 nchini Congo kwa mwaka huu waliokumbwa na migogoro ya kibinadamu inayosababishwa na migogoro ya kikabila na wanamgambo na kurejesha kumbukumbu mbaya ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ya mwaka 1998-2003.

Katika mkutano wa wafadhili wiki iliyopita, wafadhili wa kimataifa waliahidi dola milioni 528 kuelekea juhudi hizo, ikiwemo kuwapatia chakula watoto milioni 2.2 wanaokabiliwa na utapiamlo mkali na kuwafanya kuwa katika hatari ya kifo kutokana na maradhi hayo.

Kwenye taarifa yake baraza la mawaziri la Congo limesema kwamba shirika jipya la mfuko wa usimamizi wa misaada ya kibinadamu, litakuwa na jukumu la kusimamia, kufuatilia na kudhibiti misaada ya kiutu na kufanyia kazi njia zote za  mtiririko wa fedha unaoathiri sekta ya kibinadamu katika nchi.

Schweiz Geberkonferenz für DR Kongo in Genf (picture-alliance/dpa/BELGA/E. Lalmand)

Sehemu ya wajumbe waliohudhuria mkutano wa kuisadia Congo

Haikuwa wazi ni namna gani mfuko huo utafanya kazi, ikiwa wafadhili wa kimataifa watakubali kutuma fedha kwenye akaunti inayoendeshwa na serikali ya Kinshasa na ikiwa mfuko huo mpya utahatarisha fedha zilizokwisha kubaliwa chini ya sheria za nyuma.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema wanasubiri ufafanuzi wa kina kutoka serikali ya Congo kabla ya kutoa kauli juu ya hilo. Hata hivyo, uamuzi wa kubadili namna inavyopokea ufadhili, umekuja wakati sio mzuri kwa taifa hilo la afrika ya kati mzalishaji wa shaba.

Uamuzi wa rais Joseph Kabila kukataa kuondoka madarakani wakati muhula wake ulipomalizika mwaka 2016, umesababisha kuvunjika kwa mamlaka hususan maeneo mengi ya ndani ya mashariki mwa Congo, na kuongeza umri katika mgogoro wa zamani uliochangia watu milioni 4.3 kuyakimbia makazi yao.

Uamuzi huo pia unakwenda sambamba na kudhoofika kwa mahusiano ya Congo na jumuiya ya kimataifa uliochangiwa na uamuzi wa Kabila wa kukataa kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa wa wafadhili uliofanyika mjini Geneva wiki iliyopita.

Kinshasa imekataa kuwepo na mgogoro wa kibinadamu katika taifa hilo kubwa la Afrika ya Kati na kuyatuhumu mataifa ya kigeni kwa kuishutumu nchi hiyo na kuharibu uwekezaji.

CHANZO: DW-IDHAA YA KISWAHILI

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Ujumbe wa usalama wa UN washambuliwa Douma
Ujangili wapungua nchini kwa asilimia 50

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise