Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Hakuna mrithi wa Rais Xi Jinping wakati viongozi wapya…

  • October 25, 2017
Rais Xi Jinping na wanachama wa kamati kuu.

China imetangaza kamati mpya ya viongozi wakuu na kuachana na mila ya kutomtangaza mrithi wa rais Xi Jinping.

Kutotangazwa mrithi kunaashiria kuongezeka ushawishi wa Xi madarakani katika kipindi cha miaka mitano inayokuja, siku moja baada ya jina lake kujumuishwa katika katiba.

Uteuzi huo ulifanywa kwa kamati ya watu inayojulikana kama Politburo, ambayo ina nguvu zaidi nchini China.

Kamati hiyo mpya ilizinduliwa kwenye ukumbi mashuhuri wa watu wa China.

Kando na Xi mwenye umri wa miaka 64, waziri mkuu Li Keqiang, 62, ndiye mwanachama pekee wa kamati ambaye alidumisha nafasi yake.

Viongozi wa China miongo ya hivi karibuni wamekuwa wakimteua mrithi mmoja ua kadhaa katika kamati kuu, wakati wa kuanza kwa muhula wa mwisho kuonyesha warirhi watakaochukua usukani.

Viongozi wapya nchini China

kumekuwa na uvumi kuwa Bw Xi anaweeza kuwainua wanachama Chen Miner na Hu Chunhua, wote ambao wana umri wa miaka ya 50 kuweza kuwa warithi wake.

Kamati kuu ya kijehi nayo ilitangazwa. Itaongozwa na Xu Qiliang ambye anadumisha cheo hicho na Zhanga Youxia mshirika waa karibu wa Bw. Xi.

Wajumbe pia waliteua kamati kuu ya nguvu ya wanachama 200 ambao hukutana mara mbili kwa mwaka.

Mashirika ya habari ya kimataifa likiwemo la BBC yalinyimwa vibali vya kuingia ukumbi wa matangazo.

Hatua ya kutoteuliwa kwa warithi wa kamati kuu inampa nguvu zaidi Bw Xi katika miaka mitano inayokuja na kuashiria kuendelea kuwepo kwake baada ya mwaka 2022.

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Kwa nini Zimbabwe ina ‘Waziri wa WhatsApp’.
Iran yamhukumu kifo daktari mkaazi wa Sweden kwa ujasusi

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise