Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Jeshi la Zimamoto lakanusha madai ya kutokupokea simu za…

  • June 5, 2018

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani TABORA limekanusha madai ya wakazi wa mjini TABORA kwamba halipokei simu za taarifa za matukio, kuchelewa kufika kwenye matukio na kuwa na idadi ndogo ya askari.

Kamanda wa kikosi cha Zimamoto na Ukoaji mkoani TABORA,KONDO MOHAMED amesema madai hayo siyo sahihi na kwamba  kikosi chake kipo makini na kinafanya kazi zake kwa taratibu zilizopo kisheria.

Ameeleza kuwa madai yanayotolewa na wakazi wa mjini hapa hayana kweli kwa sababu kikosi chake kinapokea simu  za matukio,kuwahi kwenye matukio yote na kinakwenda katika matukio hayo kikiwa na idadi ya askari waliopo kituoni kwa kila siku husika.

KONDO amesema kuwa  kwa wastani wanapokea simu 50 za matukio kwa siku,wanawahi kwenda katika matukio yote na  kwamba kwenye matukio yote kinachotakiwa ni ufanisi wa utendaji kazi na siyo idadi idadi ya askari wanaotendakazi katika matukio hayo.

Pia amesema changamoto zinazowakabili katika utendajikazi ni wananachi wasio waaminifu kutoa taarifa za uongo za matukio na miundo mbinu mibovu ya ujenzi wa majengo usiofuata taratibu za mipango miji.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri sokoni Kachoma
Vladmir Putin aizuru Austria.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…
Serikali kuwalipa fidia wananchi wa…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise