Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Sports

Messi aiokoa Barcelona Uingereza Michuano ya Ligi Kuu Barani…

  • February 21, 2018

Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi jana usiku amefanikiwa kuiokoa klabu yake kutoka kwenye kipigo kwa kuisawazishia goli 1-1 dhidi ya mabingwa wa Uingereza Chelsea kwenye mchezo wa klabu bingwa barani Ulaya.

Lionel Messi na Andres Iniesta

Goli hilo la kusawazisha la Messi limevunja rekodi mbovu ya mchezaji huyo ya kutofunga goli lolote dhidi ya Chelsea pindi timu hizo zinapokutana akiwa na timu yake kwa zaidi ya miaka 7.

Imemchukua mchezaji  huyo dakika 730 na mechi 9 kufunga bao lake la kwanza katika michuano ya Klabu Bingwa Barani Ulaya (UEFA).

Messi ambaye amekuwa yuko katika kikosi kimoja na Andres Iniesta tangu aanze kuichezea Barcelona mpaka sasa, alikuwa hajawahi kuzigusa nyavu za Chelsea, hadi Jana usiku ilipomlazimu kutumia dakika 75 uwanjani kupata goli hilo.

Iniesta ndiye aliyemsaidia Messi kufunga bao hilo kwa pasi safi ya mwisho kunako dimba la Stamford Bridge.

Goli la Chelsea lilifungwa na Willian kunako dakika ya 62 kwa shuti zuri lililopita miguuni mwa mabeki wa Barcelona.

Kwa sare hiyo Barcelona imekuwa na faida ya goli moja la ugenini, kabla timu hizo hazijakutana tena katika mchezo wa marudiano utakaochezwa kwenye Uwanja wa Camp Nou, Jumatano ya March 14 2018.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Jeshi la polisi mkoani TABORA linaendelea na uchunguzi wa matukio mawili tofauti ya kujeruhi.
Korea Kaskazini ilivyoufuta mkutano wa makamu wa rais wa Marekani Mike Pence

Related articles

Simba Yamsajili Adam Salamba.
Roman Abrahamovich ahamia Israel.
Kipa wa Liverpool atishiwa maisha.
Haji Manara, Simba na Yanga…
Serengeti Boys wa Tanzania watwaa…
Wachezaji wanajua umuhimu wa mechi…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise