Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Moto wateketeza nyumba nyingi mtaa wa Kijiji, Nairobi

  • January 29, 2018

Mamia ya watu wamekesha nje usiku wa kuamkia leo Jumatatu, bila ya kuwa na mahali pa kulala, nchini Kenya, baada ya moto mkubwa kuteketeza nyumba zao katika mtaa wa Kijiji eneo la Langata, Nairobi.

Moto huo ambao chanzo chake

 bado hakijabainika ulizuka mwendo wa saa mbili jioni na kuenea kwa haraka.

Magari manne ya wazima moto yalifika eneo hilo kujaribu kuuzima moto huo lakini hazikuweza kuufikia kutokana na njia nyembamba mtaani humo.

Magari hayo yalijaribu kuuzima moto huo kutoka mbali lakini baadaye yakaishiwa na maji.

Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Taifa ya Kukabiliana na Majanga anayeangazia mawasiliano Bw Pius Masai aliambia gazeti la kibinafsi la Nation kwamba walilazimika kuomba usaidizi zaidi.

Magari ya kuzima moto ya baraza la jiji yalifika baadaye, lakini wakazi waliwalaumu maafisa hao wa serikali kwa kuchelewa kufika eneo la mkasa.

Moto huo baadaye ulizimwa, ingawa moshi bado ulikuwa unafuka katika baadhi ya maeneo asubuhi.

Wakazi waliambia vyombo vya habari kwamba walipoteza mali ya mamilioni ya pesa, badhi wakipoteza biashara zao na wengine makazi.

 

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Sababu ya Donald Trump kujibizana na mwanamuziki Jay-Z
TABORA: Umeme warahisisha Maisha SIKONGE.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise