Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Mwanajeshi wa Marekani aliyehamia Korea Kaskazini afariki

  • December 12, 2017

Mwanajeshi wa zamani wa Mareknai ambaye alihamia Korea Kaskazini na kuwa mfungwa kwa karibu miaka 40 amefariki.

Charles Jenkins, 77, aliishi nchini Japan ambapo alihamia na familia yake baada ya kuachiliwa mwaka 2004.

Alikuwa miongoni mwa wanajeshi wanne wa Marekani ambao walihamia Korea Kaskazini miaka ya sitini na kuwa manyota wa filamu nchini humo lakini ni yeye pekee aliweza kuachiliwa.

Wengine waliripotiwa kufariki wakiwa nchini Korea Kaskania akiwemo James Dresnok ambaye aliropitiwa kufariki kutokana na ugonjwa wa kiharusi mwaka 2016.

Charles Jenkis alifariki akiwa kisiwa cha Sado siku ya Jumatatu ambapo alikuwa akiishi na mke wake Hitomi Sofa ambaye pia ni mfungwa wa zamani wa Korea Kaskazini.

Bw. Jenkins alikuwa akiishi maisha magumu akiwa nchini Korea Kaskazini ambayo alikuja kuyaelezea baadaye kwenye mahojiano kadhaa.

Mwaka 1965 akiwa na kikosi cha Marekani nchini Korea Kusini kilichokuwa eneo la mpaka wenye ulinzi mkali, Jenkins aliamua kukihama kikosi chake na kuhamia Korea Kaskazini akihofia kuwa angeua wakati wa doria au kutumwa kupigana vita huko Vietnam.

Alisema alifikiri kuwa akiwa nchini korea Kaskazini, akangeweza kuomba hifadhi kwenye ubalozi wa Marekani na baadaye kurudi Marekani wakati wa kubadilshwa kwa wafungwa.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Miili ya wanajeshi waliouawa DRC yarejeshwa Tanzania.
Trump matatani ukatili wa kijinsia

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise