Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Ofisa Ardhi wilaya ya NAMTUMBO apewa mwezi mmoja kufidia…

  • November 24, 2017

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA amempa mwezi mmoja Ofisa Ardhi wa wilaya ya NAMTUMBO Bwana MAURUS YERA awe ametafuta ardhi ya kuwafidia wakazi wa kijiji cha LWINGA wilayani humo.

Wakazi hao 21, mwaka 2008 eneo lao lenye ukubwa wa ekari 101 lilichukuliwa na Serikali kupitia halmashauri ya wilaya hiyo kwa ajili ya kupisha ujenzi wa shule ya sekondari ya mkoa wa RUVUMA na waliahidiwa kulipwa fidia.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo alipozungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo wa LWINGA akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani RUVUMA.

 

Ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi hao kupitia mabango, ambapo wamemuomba awatatulie kero hiyo ya madai ya fidia ya ardhi iliyodumu kwa miaka 10 bila kupatiwa ufumbuzi.

Waziri Mkuu amesema haoni sababu ya Halmashauri hiyo kushindwa kuwafidia wananchi hao sehemu ya ardhi kwa muda wote huo ukizingatia wilaya hiyo ina hifadhi ya ardhi.

Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Daktari John Magufuli inataka kila mtumishi ahakikishe anatumia taaluma yake vizuri kwa kuwahudumia wananchi ikiwa ni pamoja na kutatua kero zinazowakabili kwa wakati.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Wajawazito mkoani TABORA watakiwa kuwahi kliniki mara tu wanapokuwa katika hali hiyo kutambua ugonjwa wa kifafa cha mimba.
TABORA: Wanafunzi WANNE wa kidato cha kwanza wa shule ya sekondari IKOMWA wahindwa kuendelea na masomo baada ya kugundulika kuwa ni wajawazito.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise