Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Sports

Serengeti Boys wa Tanzania watwaa ubingwa Cecafa U17

  • April 30, 2018

Timu ya Tanzania ya vijana wasiozidi umri wa miaka 17 ndio mabingwa wa Kombe la Vijana la mataifa ya Afrika Mashariki na Kati Cecafa wa mwaka 2017.

Serengeti Boys walitwaa ubingwa baada ya kuwalaza Somalia mabao 2-0 katika mechi ya fainali iliyochezewa mjini Bujumbura, Burundi.

Mabao ya Serengeti yalitiwa kimiani na Edson Jeremiah na Japhary Mtoo.

Ushindi huo ndio wa kwanza tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo mwaka 2007 na unatarajiwa kuwatia moyo vijana hao wanapijiandaa kushindi michuano ya Kombe la Vijana Mabingwa Afrika mwaka 2019.

Serengeti Boys walianzisha kampeni yao baada ya kutoka sare 1-1 na Uganda mechi yao ya kwanza lakini mechi ya pili wakalaza Sudan 6-0 uwanja wa Muyinga mjini Bujumbura.

Nusufainali, Serengeti walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kenya katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa Muyinga.

Somalia walifika fainali kwa kulaza Kenya 1-0 katika moja ya mechi zao za hatua ya makundi.

Zanzibar walidaiwa kuwasilisha wachezaji 12 wasiohitimu kucheza na wakaondolewa kwenye michuano hiyo na kutozwa faini ya Sh1.5 milioni.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Uzalishaji wa zao la Nazi washuka Zanzibar.
Wakimbizi wa Rohingya wataka ulinzi wa Umoja wa Mataifa

Related articles

Simba Yamsajili Adam Salamba.
Roman Abrahamovich ahamia Israel.
Kipa wa Liverpool atishiwa maisha.
Haji Manara, Simba na Yanga…
Wachezaji wanajua umuhimu wa mechi…
Roma yaichapa Barcelona, Yatinga nusu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise