Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Shambulio la risasi laua 17 shuleni Marekani

  • February 15, 2018

Watu 17 wameuawa katika mauaji ya watu wengi yaliyofanywa katika shule moja huko Florida Marekani.

Kwa mujibu wa polisi, mtuhumiwa huyo ametajwa kwa jina la Nikolaus Cruz mwenye umri wa miaka 19 na kwamba alikuwa mwanafunzi katika shule hiyo aliyoishambulia.

Mshambuliaji huyo ambaye alikuwa amebeba bunduki ya kisasa, alianza kushambulia bila ya mpangilio nje ya shule hiyo kabla ya kushambulia ndani, hali ambayo ilisababisha wanafunzi, kuhangaika huku na kule kwa lengo la kujificha chini ya madawati na maeneo mengine.

Kamanda wa polisi katika eneo hilo, amesema mshambuliaji huyo alifukuzwa shule kutokana na utovu wa nidhamu.

Na Tayari polisi walimkamata karibu na mji wa jirani wa Coral Springs.

Shirika la Upelelezila Marekani FBI limesema linashirikiana na polisi, kufanyia uchunguzi tukio hilo.

Shambulio hilo ni kubwa katika siku za hivi karibuni, tangu lile lililoua watu 20, katika shule ya Connecticut 2012.

Katika hatua nyingine, kupitia mtandao wake wa Tweeter, Rais Donald Trump amewaondolea hofu raia, kwa kusema kuwa usalama upo kwa mtoto, mwalimu ama mwingine yoyote yule.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mjini TABORA-TUWASA kufikisha huduma ya maji safi MALOLO.
Lupita: Sikuwahi kusikia hata filamu moja ya ushujaa yenye watu weusi

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise