Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Agizo la Rais Daktari JOHN POMBE MAGUFULI kuhusu…

  • December 14, 2017

Bodi ya Filamu katika halmashauri ya manispaa ya TABORA imepanga kukutana kuweka mikakati ya kusimamia maadili ya uvaaji kwa wasanii wa kizazi kipya baada ya Rais Daktari JOHN POMBE MAGUFULI kuagiza taasisi zinazohusika kusimamia uvaaji kwa wasanii wa kike.

Katibu wa Bodi ya Filamu wa wilaya ambaye ni Afisa Utamaduni wa manispaa ya TABORA,MEDERICKO KATUNZI amesema atazungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu ili kupanga namna watakavyosimamia maadili ya mavazi ya wasanii wa kike.

KATUNZI ameongeza kuwa manispaa ya TABORA imekuwa na wasanii chipukizi ambao wanaiga mavazi ambayo yanaacha wazi viungo vyao vya mwili jambo ambalo ni la aibu katika jamii.

Nao baadhi ya wasanii mjini TABORA, KULWA, KASELE RAMADHANI,ANASTAZIA LINUS na  RASHIDI MAGEDULA  wamesema agizo la Rais MAGUFULI  kwa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi mapema wiki hii  kuhusu uvaaji wa  nusu uchi kwa wasanii wa kike lipo sahihi kutokana na wasanii kukubuhu na uvaajihuo usiofaa.

Naye mmoja wa wakazi wa Manispaa ya T ABORA,FABIANO ALFRED amesema wasanii hawana budi kubadilika katika uvaaji wao kwa sababu wao ni kioo cha jamii na pale wanapokwenda kinyume na maadili wanapotosha umma.

Akufungua mkutano mkuu wa tisa wa Jumuiya ya Wazazi  ya Chama cha Mapinduzi,Jumanne wiki hii mjini DODOMA Mwenyekiti wa Chama hicho, Rais  MAGUFULI alieleza kukerwa kwake na Mamlaka zinazohusika na maadili kutochukua hatua dhidi ya wasanii wanaoimba majukwani wakiwa na mavazi ya nusu uchi na kumtaka Mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo kuhakikisha anasimamamia maadili ya vijana na Taifa kwa jumla.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Maelfu wakimbia vita Jamhuri ya Afrika ya Kati
TABORA: Wananchi washauriwa kutumia maji safi na salama ili kujiepusha na magonjwa ya tumbo.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise