Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

TANESCO mkoa wa TABORA yalalamikiwa kwa kushindwa kushiriki kikamilifu…

  • November 20, 2017
Mtoto Abdulkarim Ibrahim.

Shirika la umeme nchini-TANESCO mkoa wa TABORA limelalamikiwa kwa kushindwa kushiriki kikamilifu katika matibabu ya mtoto ABDULKARIM IBRAHIM aliyepigwa na shoti ya umeme katika mtaa wa MAJENGO,kata ya IPULI mjini TABORA.

Akizungumza na CGFM,Baba mzazi wa ABDULKARIM,IBRAHIM ABDALAH amesema tangu mtoto wake apigwe na shoti ya umeme tarehe 12 mwezi uliopita TANESCO haijashiriki ipasavyo hadi imefikia hatua ya mtoto huyo kupewa rufaa ya kwenda katiaka hospitali ya rufaa BUGANDO jijini MWANZA.

Awali CG FM ilitaka kufahamu mazingira  ya mtoto ABDULKARIM alipigwa na shoti ya umeme ambapo baba yake mzazi anaeleza.

Kwa upande wake,Mratibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA,Kanda ya magharibi GENERAL KADUMA amesema serikali inapaswa kuona uchungu juu ya mtoto huyo.

CG FM imemtafuta Meneja wa TANESCO mkoa wa TABORA,Injinia MOHAMED ABDALLAH kuzungumzia suala la mtoto huyo,lakini alikataa kuzungumza kwa madai kwamba suala hilo lipo kwenye uongozi wa juu yaani Makao Makuu ya TANESCO DAR ES SALAAM.

Naye Katibu wa mbunge wa viti maalum-CHADEMA,KWANDU MPANDUJI amesema mbunge wa viti maalum,HAWA MWAIFUNGA amemsafirisha mtoto ADBULKARIM kwenda BUGANDO kwa matibabu zaidi.

Tarehe 12 mwezi uliopita mtoto ABDULKARIMU IBRAHIM alipigwa shoti ya umeme wakati akienda shuleni baada ya kukuta nguzo ya umeme imeanguka na kushika nyaya zikiwa na umeme hali iliyosababisha mtoto huyo kukatwa mkono wake wa kulia baada ya kubainika mkono huo hauwezi kufanya kazi tena.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Mahakama Kenya yatupilia mbali kesi zilizopinga ushindi wa Kenyatta.
Vilabu vinavyoshiriki ligi ya mkoa wa TABORA kutoka wilaya ya UYUI  vimehakikishiwa kupewa ushirikiano.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise