Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Uchaguzi Kenya 2017: Mahakama ya Juu kusikiliza kesi muhimu

  • October 25, 2017
Uchaguzi wa marudio umepangiwa kufanyika kesho Alhamisi.

Mahakama ya juu nchini Kenya leo Jumatano itasikiliza kesi ya dharura iliyowasilishwa na wapiga kura watatu dakika za mwisho wakidai kuwa Kenya haiko tayari kufanya uchaguzi huo.

Mahakama imeombwa kuingilia kati na kuamua – iwapo uchaguzi wa marudio utafanyika..

Wanataka uchaguzi huo uahirishwe.

Rais Uhuru Kenyatta anasema uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa siku ya Alhamisi.

Muungano wa upinzani chini ya kinara Raila Odinga umetaka wafuasi wake wasusie zoezi hilo, ukiutaja kuwa uchaguzi usioweza kuwa wa huru na wa haki.

Odinga amesema Serikali ya Kenya na tume ya Uchaguzi zimeshindwa kushughulikia mapungufu yaliyosababisha mahakama ya juu zaidi nchini humo kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi Agosti.

Hatua hiyo inajiri baada ya mahakama hiyo kufanya uamuzi wa kihistoria ilipofutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais na kutaka uchaguzi huo kurejelewa.

Kuna utata kati ya sheria za uchaguzi, katiba na vile mahakama ilivyofafanua sheria hizo.

Mahakama ya juu imekubali kusikiliza ombi hilo la muda wa lala salama ambalo linahoji iwapo tume ya uchaguzi na mwenyekiti wake wataweza kufanya uchaguzi ulio huru na haki siku ya Alhamisi.

Kumeshuhudiwa maandamano ya wafuasi wa upinzani wanaopinga uchaguzi huo wa marudio na wanashinikiza maguezi ndani ya tume ya uchaguzi IEBC na pia katika mfumo wenyewe wa uchaguzi.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Iran yamhukumu kifo daktari mkaazi wa Sweden kwa ujasusi
Ukweli kuhusu Bella wa Yamoto Band kudaiwa kufunga ndoa

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise