Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Wachezaji wanajua umuhimu wa mechi dhidi ya Welayta Dicha-…

  • April 17, 2018

Wakati Young Africans SC ikielekea kwenye mchezo wake wa kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya timu ya Welayta Dicha hapo kesho siku ya Jumatano Katibu Mkuu wa Klabu hiyo, Charles Boniface Mkwasa  amesema kuwa wachezaji wanafahamu umuhimu wa mechi na wanajua matokeo kama watapata matokeo mazuri  wataelekea kwenye hatua ya makundi licha ya kuwa lolote linaweza kutokea.

Yanga SC yawapa raha Watanzania Taifa

“Wachezaji wanafahamu umuhimu wa mechi na wanajua matokeo yake wakipata matokeo mazuri  wataelekea kwenye hatua ya makundi, na wao pia wapo kwenye matarajio hayo kama unavyojua mpira hautabiriki sana kama unakumbuka Barcelona walishinda kwake tatu lakini wenzao waliyarudisha na kisha wakatoka kwahiyo lolote linaweza kutokezea kwahiyo wachezaji wangu wanatahadhari kubwa kwakuamini mechi itakuwa ngumu lakini wanamatumaini makubwa kwafaida ya Watanzania wote.”

Mkwasa ameongeza kuwa “Tumewafatilia Welayta Dicha FC wakiwa nyumbani wapoje tunajua mpira wa Ethiopia na mashabiki wanajulikana wenzetu wanakuwa na umoja sana wanapokuwa nyumbani tofauti na sisi huku tunajua tutakutana na hilo pia na sisi wapo wenzetu ambao wameshakwenda huko kusapoti vijana.”

“Matarajio ni kusonga mbele kama unavyojua unapokuwa unacheza Ligi ili kupata wawakilishi kwahiyo sisi ni wawakilishi kwahiyo mechi yetu hii ni kama tupo kwenye kipindi cha pili maana cha kwanza tumeshaongoza kwa bao 2 – 0 kwahiyo tunachotakiwa ni kuongeza moja au kulinda ushindi wetu.”

Kwenye mchezo wa awali uliyopigwa jijini Dar es salaam mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara Yanga SC walifanikiwa kuchomoza na ushindi wa mabao 2 – 0 dhidi ya Welayta Dicha magoli yaliyofungwa na Raphael Daudi sekunde 30 tu tangu mpira kuwanza na Emmanuel Martin aliepachika dakika ya 54 ya kipindi cha pili.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Wanariadha wengine watano wa Afrika wametoweka Gold Coast
Mwakyembe aagiza Nandy akamatwe, Diamond bado anahojiwa na polisi kwa kusambaza video chafu.

Related articles

Simba Yamsajili Adam Salamba.
Roman Abrahamovich ahamia Israel.
Kipa wa Liverpool atishiwa maisha.
Haji Manara, Simba na Yanga…
Serengeti Boys wa Tanzania watwaa…
Roma yaichapa Barcelona, Yatinga nusu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise