Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Walemavu wa Ngozi mkoani TABORA watakiwa kushiriki katika huduma…

  • November 22, 2017

Watu wenye ulemavu wa ngozi-ualbino mkoani TABORA wametakiwa kushiriki katika huduma za kliniki kwa ajili ya kupewa elimu sahihi ya matumizi ya mafuta ya kujikinga na mionzi ya jua na jinsi ya kukabiliana na ugonjwa wa saratani ya ngozi.

Rai hiyo imetolewa na Mratibu wa huduma za afya kutoka shirika la STANDING VOICE,KABALA MAGANJA akisema watu wanaoishi karibu na kliniki za matibabu ya watu wenye ualbino  watumie fursa hizo kenda vituoni ili watibiwe.

Katika hatua nyingine ameitaka jamii kutambua umuhimu wa watu wenye ualbino kwa kuwa mstari wa mbele kupinga mauaji na hata kuwapatia elimu watoto wenye ualbino.

Kwa upande wake,Katibu wa chama cha watu wenye ualbino mkoa wa TABORA RAMADHANI MLAMBA amewasihi watu wenye ualbino kujitokeza kwa wingi katika kliniki hizo na matibabu ili waweze kujua njia sahihi za kukabiliana na magonjwa mbalimbali.

Shirika la STANDING VOICE linatoa huduma kwa watu wenye ualbino katika vituo vitano Mkoani TABORA ambavyo ni Hospitali ya rufaa ya mkoa wa TABORA-KITETE,shule ya msingi FURAHA, shule ya sekondari TABORA WASICHANA,Hospitali ya wilaya ya NZEGA na Hospitali ya wilaya ya URAMBO.

Katika zoezi hilo la utoaji wa huduma kwa watu wenye ualbino ambalo limeanza kutolewa katika vituo hivyo linaambatana na utoaji wa elimu,vifaa kama kofia,miwani na mafuta ya  kupaka ili ya kujikinga na mionzi ya jua kwa lengo la kuzuia saratani ya ngozi kwa watu hao.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

BAADA YA JANGA LA MOTO, CLOUDS MEDIA GROUP YAKUMBANA NA FAINI YA MILIONI 12.
Tatizo la uchumi na uelewa mdogo ni moja ya sababu zinazopelekea baadhi ya wazazi kukatisha ndoto za watoto wao.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise