Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Wamiliki wa Mabasi, Madereva na Abiria watakiwa kutii kanuni…

  • May 16, 2018May 16, 2018

Wamiliki wa mabasi,madereva na abiria wametakiwa kutii sheria na kanuni za usafirishaji ili kupunguza kero na kadhia kwa abiria.

Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Usafirishaji wa Majini na Nchi Kavu – SUMATRA,JOSEPH MICHAEL amesema watu WATATU wamekamatwa kwa kukiuka kanuni ya 23 ya usafirishaji ambayo inakataza kufanya biashara,mahubiri na burudani ndani ya mabasi.

Ameongeza kuwa wakati wote wa safari kwa mujibu wa kanuni ya usafirishaji, mmiliki wa basi ambaye kwa wakati huo ni dereva na kondakta watawajibika iwapo watakiuka kanuni hiyo.

Kwa upande wake, Mjumbe wa Kamati ya Usalama Barabarani,Manispaa ya TABORA,IBRAHIM WAZIR I amesema kuwa kuwepo kwa kanuni za usafirishaji  kumepunguza vitendo vya wizi kwa sababu baadhi ya wafanyabiashara wanaoingia kwenye mabasi hayo siyo waaminifu.

Kwa mujibu wa kanuni ya 23 ya usafirishaji ya mwaka 2017 kifungu B pia kinaeleza kwamba  mtu kufanya biashara,siasa,kuhubiri au kutoa  burudani ndani ya magari ya abiria ni kinyume cha kanuni hiyo.

Mwandishi: NAJJATH OMAR, CG FM.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Milioni 334 zatengwa kwa ajili kuzigawa kwenye vikundi vya wanawake.
Watu milioni 12 duniani kote ni wakimbizi wa ndani.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise