Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Wananchi wametakiwa kuepuka matumizi ya bidhaa za vyakula na…

  • October 9, 2017
Wananchi wametakiwa kuepuka matumizi ya bidhaa za vyakula na dawa zilizopita  muda wake.

Wananchi wametakiwa kuepuka matumizi ya bidhaa za vyakula na dawa zilizopita  muda wake wa matumizi pamoja na vipodozi vyenye viambata sumu ili kujiepusha na madhara wanayoweza kumpata mtumiaji.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Mamlaka ya chakula na dawa Kanda ya Magharibi Dakta EDGER MAHUNDI, katika zoezi la kuharibu bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu, tani 17.5 zenye thamani ya shilingi milioni 55.

Amesema bidhaa  hizo zimekamatwa katika mikoa ya TABORA, KIGOMA na KATAVI na kwamba mamlaka hiyo ina jukumu la kukagua maeneo yote yanayojihusisha na bidhaa wanazodhibiti kwa kushirikiana na maafisa wa afya na wafamasia.

Afisa Afya Mkuu Manispaa ya TABORA PASCHAL MATAGI amewashauri wananchi watumie bidhaa zilizoandikwa kwa lugha wanazozielewa kama vile Kingereza na Kiswahili.

Mamlaka ya chakula na dawa TFDA imewasisitiza kujali afya zao, kwa kuzingatia  matumizi sahihi ya bidhaa na kuwafichua wafanyabiashara wanaoingiza bidhaa kwa kutumia njia za panya.

Amesema bidhaa  hizo zimekamatwa katika mikoa ya TABORA, KIGOMA na KATAVI na kwamba mamlaka hiyo ina jukumu la kukagua maeneo yote yanayojihusisha na bidhaa wanazodhibiti kwa kushirikiana na maafisa wa afya na wafamasia.

Licha ya uwezo wa kiuchumi kuwa mdogo kwa baadhi ya wananchi, Mamlaka ya chakula na dawa TFDA imewasisitiza kujali afya zao, kwa kuzingatia  matumizi sahihi ya bidhaa na kuwafichua wafanyabiashara wanaoingiza bidhaa kwa kutumia njia za panya.

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Watu 12 wa Rohingya wafa maji wakijaribu kuvuka kwenda Bangladesh.
Jackie Chan athibitisha ujio wa filamu ya ‘Rush Hour 4’

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise