Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Watu wawili wamekufa katika matukio mawili tofauti Mkoani TABORA

  • December 27, 2017

Kamanda wa polisi mkoa wa TABORA kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi WILBROAD MUTAFUNGWA amesema tukio la kwanza limetokea katika wilaya ya IGUNGA ambapo MIPAWA LUFUNGA ameuawa kwakuchomwa kisu.

Amesema kufuatia tukio hilo wananchi kwa kushirikiana na jeshi la polisi wamemtia mbaroni mtuhumiwa huyo na anaendelea kuhojiwa katika kituo cha polisi IGUNGA na uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.

Katika tukio jingine Kamanda MUTAFUNGWA amesema mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la MICHAEL PETER mkazi wa kata ya CHEMCHEM amegundulika amekufa kwenye kilabu cha pombe za kienyeji mtaa wa MASEMPELE kata ya NGAMBO Manispaa ya TABORA.

Awali akizungumzia tukio hilo Mwenyekiti wa mtaa wa MASEMPELE kata ya NG’ AMBO SHABAN KAOMBWE amekiri kuwa alipata taarifa za tukio hilo mapema na alitoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa msaada zaidi.

Kwa upande wake mjumbe wa serikali ya mtaa wa MASEMPELE NASORO JUMA amesema mtaa huo unaongoza kwa matukio ya mauaji hivyo ameiomba serikali iwasaidie kutokana na mtaa huo kuwa na vijana wengi wanaocheza kamali.

Kwa mujibu kamanda wa polisi mkoa wa TABORA wana mkakati wa kuangalia mambo yanayochangia matukio ya kihalifu hasa ya utengenezaji na utumiaji wa pombe za kienyeji ikiwemo gongo

Na wanaendelea na misako ili kuhakikisha wananchi wanakunywa pombe zilizopimwa na kukaguliwa na shirika la viwango nchini TBS.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Obama aonya kuhusu matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii
Wimbo wa ‘Kivuruge’ wamgusa Naibu Spika

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise