Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Wazazi husababisha watoto kutosoma vizuri na usumbufu kwa walimu…

  • January 9, 2018

Wazazi wanaochelewa kuwapeleka watoto wao shule zinapofunguliwa  wanasababisha wanafunzi kutosoma vizuri darasani na kuleta usumbufu kwa walimu.

Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi ISIKE katika halmashauri ya Manispaa ya TABORA,PAUL SONGORO amesema mahudhurio ya wanafunzi siku ya kwanza siyo ya kuridhisha kutokana na wazazi kuwasafirisha watoto wao kwenda mbali wakati wa likizo.

Kwa upande wake,Mwalimu wa taaluma katika shule hiyo ya msingi,MARIAM JONATHAN amesema licha ya mahudhurio siku ya kwanza kuwa ya wastani lakini walimu wameanza rasmi kufundisha.

Hata hivyo wamewapongeza wazazi wa wanafunzi waliohudhuria masomo kwa sababu wamejitahidi kuwanunulia sare za shule,madaftari na viatu na kuwataka wazazi wengine waige mfano huo.

Baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba waliokuwepo shuleni siku ya kwanza baada ya shule kufunguliwa TAUSI MUSA na ANANIA PIUS wamesema wamejiandaa vyema kukabiliana na mitihani iliyoko mbele yao.

Uongozi wa shule ya msingi ISIKE unatarajia kuitisha kikao cha wazazi baadaye wiki hii ili kuweka mipango madhubuti ya wanafunzi kupata chakula shuleni hatua ambayo itaongeza uelewa kwao na kupunguza utoro.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Australia inataka kuwa muuzaji mkubwa wa bangi duniani
Halmashauri ya Manispaa ya TABORA wamezungumzia changamoto za uvunaji wa maji ya mvua .

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise