Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Zaidi ya shilingi Bilioni 23 na Milioni 200 zimetumika…

  • October 25, 2017
Tasaf.

Zaidi ya shilingi Bilioni 23 na Milioni 200 zimetumika kunusuru kaya maskini na miradi mbalimbali ya maendeleo kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii nchini- TASAF)

Mratibu wa TASAF mkoa wa TABORA,NGOKO BHUKA katika taarifa yake kwa viongozi wa TASAF makao makuu amesema fedha hizo zimetumika kuanzia mwaka 2015 hadi Agosti mwaka huu.

Amesema wilaya ya UYUI ndiyo imenufaika zaidi kwa kupata zaidi ya shilingi milioni 562.

Naye Mratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii wilaya ya UYUI,Daktari SHIJA MAIGE amesema kuwa fedha zote zilizotolewa na TASAF zilifika kwa walengwa kwa muda muafaka na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya wilaya hiyo huku akiomba walionufaika na mpango wa TASAF kutoondolewa kwenye mpango baada ya kuondokana na umaskini.

Akitoa maelekezo juu ya fedha hizo kuendelea kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa, mtaalam wa mafunzo na ushirikishwaji kutoka TASAF Makao Makuu,MECRY MANDAWA  amesema TASAF ina lenga kuinua kaya maskini na kutekeleza miradi ya maendeleo.

Naye Afisa Uwasilishaji Fedha,KWEJI KASULENDE amesema TASAF inakusudia kuinua zaidi vikundi vya wajasiriamali pamoja na vikoba ili kkufikia malengo yaliyokusudiwa.

Viongozi wa TASAF Makao Makuu wako katika ziara ya siku tatu mkoani TABORA  kukagua miradi mbali mbali inayotekelezwa kwa fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii nchini.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Wakuu wa shule zote za sekondari mkoani TABORA wametakiwa kusimamia nidhamu kwa wanafunzi bila kukata tamaa .
Wananchi wa Kata ya Loya Wilaya ya Uyui Mkoani TABORA Waomba kupunguzwa kwa Masharti na vigezo ili waweze kufungua kitui cha Polisi.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise