Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Wadukuzi wa Korea Kaskazini wadukua kampuni ya televisheni Uingereza

  • October 17, 2017October 17, 2017
Mwandishi wa Opposite Number Matt Charman.

Wadukuzi wa Korea Kaskazini wamelenga kampuni moja ya vipindi televisheni nchini Uingereza ambayo inatengeneza kipindi wa kuigiza kuhusu nchi hiyo.

Kipindi hicho ambacho kilitarajiwa kuandikwa na mwandishi ambaye ashateuliwa kuwania tuzo za Oscar sasa kimesitishwa.

Mwezi Agosti mwaka 2014 Channel 4 ilitangaza kuwa kipindi hicho kitakuwa kipya na cha kuchokoza.

Kipindi hicho kinachojulikana kama Opposite Number, kinahusu mwanasayansi ya nyuklia muingereza ambaye amefungwa nchini Korea Kaskazini.

Rais wa Korea Kaskazini akionekana katika Televisheni

Kompiuta za kampuni husika za Mammoth Screen zilidukuliwa.

Mradi huo haujapiga hatua kutokana na kushindwa kupata ufadhili kwa mujibu wa kampuni hiyo.

Maafisa wa Korea Kaskazini walijibu kwa hasira wakati taarifa kuhusu kipindi hicho zilifichuka mara ya kwanza.

Kava ya FIlamu ya Sony inayokwenda kwa jina la “The Interview”.

Pyongyang ilitoa wito kwa serikali ya Uingereza kuzima kipindi hicho ili kuzuia kuharibu uhusiano.

Korea Kaskazini kisha ikachukua hatua zaidi na kudukua kompiuta za kampuni husika.

Udukuzi huo haukusababisha uharibifu lakini, kuhusika kwa wadukuzi wa Korea Kaskazini mitandaoni kulizua hofu juu ya ni kipi wana uwezo wa kukifanya.

Hofu hiyo ilitokana sababu Sony Pictures ililengwa na udukuzi kama huo mwezi Novemba mwaka 2014.

Marekani ilisema kuwa udukuzi huo uliendeshwa na Korea Kaskazini.

Udukuzi huo nao ulikuwa ni jibu kwa filamu iliyopangwa kutolewa kwa jina The Interview, mchezo ambao kiongozi wa Korea Kaskazini aliuawa.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Leicester City 1-1 West Bromwich
MILLEN MAGESEWA AIKUMBUKA SIKU YA MAAJABU YA MTOTO WAKE WA KWANZA MAISHANI

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise