Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

ANC inamchagua kiongozi mpya Afrika Kusini.

  • December 18, 2017

Chama tawala nchini Afrika Kusini ANC kimewaidhinisha wagombea wawili kuwania kumrithi Rais Jacob Zuma katika uongozi wa chama.

Wagombea hao ni makamu wa rais Cyril Ramaphosa na waziri wa zamani Nkosazana Dlamini-Zuma, mke wa zamani wa bwana Zuma.

Kumekuwa na mvutano, hisia zikipanda, wajumbe wakipiga kelele kupinga taratibu za upigaji wa kura.

Uwaniaji madaraka umeleta mvutano mkubwa wa kisiasa, hali inayoleta hofu kuwa ANC inaweza kugawanyika kabla ya uchaguzi wa 2019.

Rais Zuma ameonya kuwa chama kimo hatarini na kimo kwenye njia panda.

Zaidi ya wajumbe 5,000 wanashiriki katika mkutano wa siku nne katika ukumbi wa Expo Centre mjini Johannesburg.

Kwa namna inavyoonekana, Bw Ramaphosa ana wafuasi 1,469 kulinganisha na 1,094 wa mke wa zamani wa Rais Zuma, Bi Dlamini-Zuma.

Lakini wengi wanasema pale ambapo matokeo yatawekwa wazi, kunaweza kuwa na tofauti nyembamba kabisa kati ya atakayeshinda na atakayeshindwa yatawekwa wazi, anaeleza Lebo Diseko mwandishi wa BBC aliyeko katika eneo la mkutano.

Rais Zuma ambaye amekuwa mamlakani tangu mwaka 2009 anategemewa kusalia uongozini hadi uchaguzi wa taifa mwaka 2019.

Afrika Kusini ina ukomo wa rais kwa vipindi viwili vya miaka mitano

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Jose Mourinho: Meneja wa Man Utd atakiwa kufafanua kuhusu Man City.
Ramaphosa ahaidi kuimarisha uchumi wa Afrika Kusini

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise