Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Baadhi ya shule Mkoani TABORA zimeweka mazingira mazuri kwa…

  • October 16, 2017
Mwalimu wa mazingira MAHALALA NICHOLAUS na mwalimu wa afya AGNESS LUGONDA wa shule ya sekondari KAZEHILI wameziomba asasi mbalimbali kuwasaidia kutoa vifaa kama pedi na dawa ambazo zitawasaidia wanafunzi watakapokuwa katika kipindi cha hedhi.

Baadhi ya shule Mkoani TABORA zimeweka mazingira mazuri kwa ajili ya wanafunzi wa kike kujisitiri wanapokuwa katika kipindi cha hedhi.

Hayo yamebainishwa na Afisa Elimu Mkoa wa TABORA Bi SUZAN NUSU akisema kuwa mikakati inaendelea kuhakikisha kila shule inakuwa na chumba maalumu kwa ajili ya wanafunzi ambao wamefikia umri wa kubalehe.

Naye Mkuu wa shule ya Sekondari KAZIMA Mwalimu MRISHO KIVURUGA amesema katika shule hiyo wanafunzi hutumia chumba cha Matroni kama chumba cha huduma ya kwanza wanapokuwa katika kipindi cha hedhi.

Kwa upande wake mwanafunzi wa darasa la sita ambaye amepewa jina la SIKUJUA KAMBA siyo jina lake halisi wa shule ya msingi CHEMCHEM Manispaa ya TABORA anaeleza adha anayopata anapokuwa katika hedhi akiwa mazingira ya shuleni.

Mwalimu wa mazingira MAHALALA NICHOLAUS na mwalimu wa afya AGNESS LUGONDA wa shule ya sekondari KAZEHILI wameziomba asasi mbalimbali kuwasaidia kutoa vifaa kama pedi na dawa ambazo zitawasaidia wanafunzi watakapokuwa katika kipindi cha hedhi.

Kwa mujibu wa mwalimu wa taaluma shule ya msingi CHEMCHEM HELENA YESSE wanafunzi wa kike hukosa masomo kutokana na tatizo la hedhi ambapo shule zimetakiwa kuweka mazingira wezeshi ili kuwasaidia wanafunzi wa kike kujistiri wakiwa kwenye hedhi.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Video Mpyaa: Harmonize ft Korede Bello – Shulala
Wananchi mkoani TABORA wametakiwa kutunza Misitu ili kupata mvua za kutosha na kuuepusha Mkoa kuingia katika janga na kukosa chakula.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise