Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

CARITAS Lakabidhi gati la maji Ndevelwa.

  • January 18, 2018

Zahanati ya kijiji cha NDEVELWA katika halmashauri ya Manispaa ya TABORA kukabidhiwa gati la maji ili kukabiliana na tatizo la ukosefu wa maji.

Idara ya Maendeleo ya Jamii ya Kanisa Katoliki –CARITAS –Jimbo Kuu la TABORA, limekabidhi gati la maji lenye thamani ya shilingi milioni 13 katika zahanati ya NDEVELWA,Manispaa ya TABORA  ili kumaliza tatizo la ukosefu wa maji katika zahanati hiyo.

Akikabidhi gati hilo kwa serikali ya kijiji cha NDEVELWA,Mkurugenzi wa CARITAS TABORA, Padri ALEX NDUWAYO amesema baada ya kugundua kuwepo kwa tatizo la ukosefu wa maji katika zahanati hiyo waliamua kutoa msaada wa kujenga gati hilo.

Kwa upande wake,Diwani wa kata ya NDEVELWA,SELEMAN MAGANGA ameishukuru CARITAS na kwamba sasa tatizo la ukosefu wa maji limemalizika kwa sababu gati hilo lina uwezo wa kuhifadhi lita elfu 55 za maji.

Naye Mganga Mfawidhi wa zahanati ya NDEVELWA,JAPHET HOSA amesema kipindi cha nyuma wagonjwa walikuwa wakilazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya maji.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa CARITAS,Idara hiyo ya maendeleo ya jamii ya Kanisa Katoliki inaendelea kushirikiana na serikali katika miradi mbalimbali ya imaendeleo ili kupunguza matatizo yanayowakabili wananchi wa TABORA.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Mafuriko yazuia wanafunzi kwenda shule.
Mgogoro wa ujenzi wa makao makuu ya wilaya ya TARIME watatuliwa.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise