Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

CHAD yamkosoa Rais DONALD TRUMP wa Marekani.

  • September 27, 2017
Rais wa Marekani Donald John Trump.

Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya CHAD imewasilisha kwa balozi wa MAREKANI malalamiko na ukosoaji wake kuhusu amri dhidi ya uhamiaji  iliyotolewa hivi karibuni na Rais DONALD TRUMP wa nchi hiyo

Mbali na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya CHAD kulalamikia hatua hiyo imemwita Balozi wa MAREKANI nchini humo,Bwana GEETA PASI na kuonyesha masikitiko yake kuhusiana na hatua ya Rais TRUMP ya kuijumuisha CHAD kupitia amri dhidi ya uhamiaji.

Kufuatia hatua hiyo serikali ya CHAD imeitaja hatua hiyo kuwa isiyo ya uadilifu na ya kushangaza.

Wizara hiyo imewahutubu viongozi wa MAREKANI ikisema uamuzi huo wa MAREKANI hauwezi kutetewa.

Awali Bwana GEETA PASI,Balozi wa MAREKANI nchini CHAD alikuwa amedai kuwa hatua hiyo ya kuijumuisha nchi hiyo ya Afrika katika amri hiyo,haitakuwa na athari  yoyote mbaya katika uhusiano wa CHAD na MAREKANI.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

TRA mkoa wa TABORA imewataka wajasiriamali kusajili biashara zao ili kuondoa usumbufu unaoweza kujitokeza wakati wa ukaguzi.
ANTONIO GUTERRES amesema lengo la dunia isiyo na silaha za nyuklia linahitaji juhudi za kimataifa

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Guardiola alinichukulia kama adui na…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise