Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

FIFA HAIMTAMBUI LUKAKU KUWA MFUNGAJI WA MUDA WOTE UBELGIJI.

  • November 16, 2017

 

Baada ya Shirikisho la Soka Duniani FIFA kufuta matokeo ya Mchezo wa kirafiki kati ya Ubelgiji dhidi ya Luxembourg hali hiyo imebadili rekodi ya Romelu Lukaku kuwa Mfungaji wa muda wa Timu hiyo.

FIFA imefuta matokeo ya mchezo huo baada ya kocha wa Ubelgiji kufanya mabadiliko ya wachezaji saba badala ya Sita ambayo ni kinyume na sheria za FIFA hivyo matokeo wala Magoli ya Mchezo huo hayatahesabika.

Mchezo huo ambao Lukaku alifunga magoli mawili katika ushindi wa magoli 5-3 na kumfanya nyota huyo kuwa na magoli 30 kabla ya kufunga goli dhidi ya Japan na kumfanya Mfungaji wa muda wote ndani ya Ubelgiji akifikisha magoli 31 lakini kwa sasa anatambulika kuwa na Magoli 28.

Mpaka sasa rekodi ya Mfungaji bora wa muda wote katika Timu ya Taifa ya Ubelgiji kwa mujibu wa FIFA inashikiliwa na Bernard Voorhoof pamoja na Paul van Himst wenye magoli 30 kila mmoja.

Lukaku atalazimika kusubiri mpaka mwezi Machi Mwakani 2018 wakati wa mechi za Mwisho kabla ya Kombe la Dunia kuanza.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Steve Nyerere amuonya Afande Sele, ‘ni uchochezi wa kuua sanaa’.
Ufaransa yamualika waziri mkuu wa Lebanon Saad Hariri.

Related articles

Mashabiki wa klabu ya YANGA…
Lagos, NIGERIA: Yemi Alade na…
STEPH CURRY aiongoza Golden State…
ShiiKANE Diamond alistahili tuzo
The Story of Adisson yaharibu…
Simba Yamsajili Adam Salamba.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise