Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi mkoani TABORA imempongeza…

  • October 25, 2017
Rais Dkt. John Magufuli alipokuwa katika moja ya mkutano wa Hadhara Mkoani Tabora.

Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi mkoani TABORA imempongeza Rais JOHN POMBE MAGUFULI kwa kazi nzuri ya kusimamia raslimali za nchi yetu na kuhakikisha zinatumika vizuri kwa manufa ya watanzania na vizazi vijavyo.

Taarifa iliyotolewa mwishoni mwa kikao chake maalum,halmashauri kuu hiyo imesema CCM mkoa wa TABORA inaunga mkono jitihada zote za serikali ya Awamu ya Tano katika kuimarisha uchumi wa nchi na kuboresha maisha ya Watanzania.

Halmashauri Kuu ya CCM hali kadhalika imempongeza Rais kwa uteuzi wa mawaziri wanaotoka mkoa huu ambao ni Dakari HAMISI KIGWANGALA- Mbunge wa NZEGA vijijini kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na JOSEPH KAKUNDA -Mbunge wa SIKONGE kuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI.

Kikao hicho licha ya kuwapongeza wabunge wote wa mkoa wa TABORA kwa jinsi wanavyotekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM pia kimewataka kuhakikisha wanatimiza ahadi zote walizoahidi wananchi wa majaimbo yao ili iwe rahisi kwa ushindi wa CCM mwaka 2019 wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na mwaka 2020 katika uchaguzi mkuu.

Chama cha Mapinduzi mkoa wa TABORA kimeipongeza serikali kwa hatua inazoendelea kuchukua katika kusimamia vyama vya msingi vya tumbaku na kupambana na vitendo vya rushwa na ufisadi.

Pia kimeitaka serikali kuharakisha mpango wa ununzi wa tumbaku ambayo bado ipo mikononi mwa wakulima ili kuwainua kiuchumi na kuwawezesha kujiandaa vizuri na msimu unaoanza wa kilimo.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Wananchi wa Kata ya Loya Wilaya ya Uyui Mkoani TABORA Waomba kupunguzwa kwa Masharti na vigezo ili waweze kufungua kitui cha Polisi.
NAIROBI, Mahakama ya Juu KENYA yashindwa kusikiliza kesi ya kuahirishwa kwa uchaguzi kutokana na ukosefu wa majaji wa kutosha mahakamani.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise