Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Halmashauri ya manispaa ya TABORA imeshindwa kukusanya asilimia 50…

  • January 30, 2018

Halmashauri ya manispaa ya TABORA imeshindwa kukusanya asilimia 50 ya mapato ya ndani katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2017-2018 na badala yake imekusanya asilimia 38 peke yake.

Akizungumza katika kikao cha mapendekezo ya rasimu ya bajeti ya mwaka ujao wa fedha wa  2018-2019  ya shilingi Bilioni 61.4,Mchumi wa Manispaa ya TABORA, JOHANNES KILONZO amesema wameshindwa kufikia lengo la ukusanyaji wa  mapato ya ndani kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake,Meya wa Manispaa ya TABORA,LEOPARD ULAYA amesema kikao cha kujadili mapendekezo ya bajeti kipo kwa mujibu wa sheria.

Naye Mkuu wa wilaya ya TABORA,Mwalimu  QUEEN MLOZI amesema katika mwaka wa fedha 2016-2017 halmashauri hiyo  ilikuwa na hoja ya kujibu na kuwataka mwaka  kuhakikisha  katika mwaka huu wa fedha wasije na majibu yale yale.

Amesema wanashikamana katika ukusanyaji wa mapato ili kufikia asilimia 80 na hivyo kusaidia kuleta maendeleo katika wilaya ya TABORA

Akizungumza katika kikao hicho,Diwani wa kata ya NG’AMBO,GEORGE MPEPO ameunga mkono kauli ya mkuu wa wilaya ya TABORA ya kuhakikisha wanaongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya TABORA limepitisha kwa kauli moja mapendekezo ya bajeti ya shilingi Bilioni 61 na milioni 400 kwa ajili ya mwaka wa fedha 2018-2019.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Bodi ya Filamu yamaliza yamaliza tofauti kati ya mtayarishaji wa filamu ya ‘Utu Wangu’ na kampuni ya Steps Ent
TABORA: Halmashauri ya Manispaa ya TABORA imeshauriwa kuweka utaratibu mzuri wa uzoaji wa taka.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise