Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Jeshi la polisi mkoani TABORA likishirikiana na Wamiliki wa…

  • December 5, 2017

Jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani mkoni TABORA limesema mpango ulionzishwa na jeshi hilo kwa kushirikiana na wamiliki wa vituo vya mafuta wa kutowapatia huduma ya mafuta waendesha pikipiki wasiokuwa na kofia ngumu utafanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Kamanda wa polisi kitengo cha usalama barabarani,Mrakibu wa polisi EMILIAN KAMUHANDA amesema wanatambua changamoto zilizopo kwa waendesha pikipiki na kwamba jeshi la polisi litafuatilia katika vituo vyote vya mafuta na kuwachukulia hatua waendesha pikipiki watakaokiuka utaratibu uliowekwa.

Amesema lengo la mpango huo ni kudhibiti ajali ambazo zimekuwa zikipoteza nguvu kazi ya taifa  na kwamba waendesha pikipiki wanapaswa kutekeleza mpango huo.

Naye mwenyekiti wa waendesha pikipiki katika kata ya KIDONGO CHEKUNDU SAIDI HAMISI amelipongeza jeshi la polisi kwa kuanzisha mpango huo na kuwasihi waendesha pikipiki wenzake kuzingatia sheria.

Nao baadhi ya waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda mbali na kupongeza mpango huo,wameliomba jeshi la polisi kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mpango huo kwa sababu kuna baadhi yao hawatekelezi.

Kwa upande wao baadhi ya wamiliki wa vituo vya mafuta mjini TABORA wamesema kuna baadhi ya bodaboda hawatekelezi agizo hilo na kwamba kutokana na maagizo ya jeshi la polisi wanagoma kuwauzia mafuta bila ya kuwa na kofia ngumu.

Tarehe mosi mwezi huu jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani mkoani TABORA kwa kushirikiana na wamiliki wa vituo vya mafuta walianzisha operesheni ya mwendesha pikipiki asiye na kofia ngumu maarufu kama Helment kutopewa  huduma ya mafuta.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Elimu ya uzazi wa mpango bado haijawafikia vijana wengi kwa sababu ya kudhani kwamba njia hizo ni kwa ajili kwa wanawake waliozaa na kudai kuwa zinasababisha Ugumba.
Kenya kuzalisha kawi ya nyuklia kufikia 2027

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise