Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Jeshi la polisi mkoani TABORA limewataka madereva kufuata sheria

  • January 11, 2018

Jeshi la polisi mkoani TABORA limewataka madereva kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamojana  na kuepuka ulevi kwani ndiyo chanzo cha ajali.

Kamanda wa polisi mkoa wa TABORA Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi WILBROAD MUTAFUNGWA amesema dereva anapotumia kilevi akiwa kazini anahatarisha maisha yake na abiria.

Pia Kamanda MUTAFUNGWA amewataka wamiliki wa vilabu vya pombe na Bar   kuzingatia muda halali wa kufanya biashara zao kama leseni zao zinavyowaelekeza.

Naye mwenyekiti wa mtaa wa MASEMPELE kata ya NG’AMBO mjini TABORA SHABAN KAOMBWE amesema kuwa kuna wauzaji wa pombe za kienyeji wasiotambulika na serikali nakuwataka wafuate sheria za biashara hiyo ikiwa ni pamoja na kuzingatia muda wa kufungua na kufunga.

Dereva wa bodaboda , PASCO JOHN  amewasihi  madereva wenzake wa vyombo vya usafiri kuwa makini na kazi zao kwa kuepuka ulevi kwani ni chanzo cha kurudisha nyuma maendeleo yao.

Hata hivyo, jeshi la polisi nchini linahimiza kila abiria kuwa na mwamko wa kutoa taarifa pindi anapobaini dereva wa chombo husika cha usafiri ametumia kilevi au anaendesha kwa mwendo kasi ili kuepuka ajali zinazoepukika.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Kesi 1197 kufikishwa ofisi ya Mkoa wa Mkoa Tabora
Daktari aelezea visababishi vya watoto kufariki tumboni.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise