Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Kamati ya Ushauri ya Manispaa ya TABORA imepitisha mapendekezo…

  • January 23, 2018

Kamati ya Ushauri ya Manispaa ya TABORA imepitisha mapendekezo ya rasimu ya mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2018-2019.

Akiwasilisha mapendekezo hayo katika kikao cha kamati ya ushauri ya manispaa ya TABORA,Mchumi wa Manispaa,JOHANNES KILONZO amesema katika mwaka wa fedha 2018-2019 jumla ya shilingi Bilioni 61 na Milioni 400 zitatumika.

KILONZO amesema mchakato wa maandalizi ya bajeti ya vyanzo vya ndani yamejikita zaidi katika michanganuo ya makisio ya vyanzo mbalimbali.

Kwa upande wake,mkuu wa wilaya ya TABORA,Mwalimu QUEEN MLOZI amewapongeza wajumbe wa kikao hicho kwa kujadili na kupitisha mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha 2018-2019.

Amewataka wajumbe wa kikao hicho kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha wanawaletea maendeleo wananchi wanaotumikia na kuachana na masuala yasiyo ya msingi.

Nao viongozi wa siasa,SAIDI LENGWE na ROBERT MHOZYA kwa pamoja wameunga mkono mapendekezo ya bajeti ya bajeti hiyo.’

Wajumbe wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Halmashauri ya Manispaa ya TABORA wameutaka uongozi wa Manispaa kuhakikisha  makabrasha ya mapendekezo ya bajeti yanawafikia mapema ili waweze kupata muda wa kutosha kuyapitia kabla ya kujayadili.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Seneti Marekani laidhinisha matumizi ya shughuli za serikali
ARUSHA :Jeshi la polisi Laanzisha Operesheni ya kukamata silaha za kijeshi zilizopo mikononi mwa wananchi.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise