Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Lupita Nyong’o; Weinstein alinifanyia unyanyasaji wa kijinsia

  • October 20, 2017October 20, 2017

Lupita amelieleza gazeti la  New York Times, kuwa amewahi kufanyiwa unyanyasaji huo na Weinstein ambaye walikutana mwaka 2011, katika sherehe za ugawaji tuzo mjini Berlin, Ujerumani kipindi bado ni mwanafunzi katika shule ya uigizaji ya Yale School of Drama.

Mrembo huyo ameeleza kuwa alitambulishwa na rafiki yake kwa Weinstein, na aliambiwa akae karibu  na mwanaume huyo ili aweze kufanikiwa katika taaluma yake uigizaji. Lupita ameeleza kuwa baada ya muda kupita alialikwa na mwanaume huyo nyumbani kwake kwa ajili ya kumuunganisha katika dili za kucheza filamu.

“Nilifika nyumbani kwa Weinstein, nikakutana na mke wake na watoto wake na kisha akaenda kuandaa chumba binafsi kwa ajili ya kutazama filamu. Baada ya dakika 15 Weinstein alirejea sebuleni na kunialika katika chumba hicho binafsi.” ameeleza Lupita.

Akaongeza “Baada ya kufika chumbani humo Harvey aliniomba nimfanyie massage, akajiandaa kwa ajili ya massage ila niliondoka chumbani na nyumbani kwake baada ya mwanaume huyo kutaka kunivua nguo zangu.”

Kufuatia tukio hilo Lupita  ilitishiwa na Weinstein, kuharibia taaluma yake ya uigizaji ila baada ya ushindi wa tuzo ya Oscar 2014, Weinstein alimfuta  muigizaji huyo na kumuomba wafanye filamu ila mrembo huyo alichomoa dili hilo.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Mesut Ozil ataka kuondoka Arsenal ajiunge na Manchester United.
Rais Magufuli ampa maagizo haya Prof. Kabudi.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Mashabiki wa klabu ya YANGA…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise