Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Maafisa ugani katika wilaya ya IGUNGA mkoani TABORA wametakiwa…

  • October 7, 2017October 7, 2017
Pamba

Maafisa ugani katika wilaya ya IGUNGA mkoani TABORA wametakiwa kuwa karibu na wakulima wa zao la pamba ili kanuni,taratibu na sheria za kilimo cha zao hilo zifuatwe.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa mkoa wa TABORA,AGGREY MWANRY wakati akizungumza na wananchi wa kata za ISAKAMALIWA,BUKOKO,MWAMASHIGA, MWAMAKONA, na ITUNDURU wilayani IGUNGA.

Nao baadhi ya maafisa ugani NCHEMBI MPEMBA wa kata ya ISAKAMALIWA na GABRIELI PAUL wa kata ya BUKOKO wamesema watasimamia vyema maelekezo yaliyotolewa na mkuu wa mkoa.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya IGUNGA,JOHN MWAIPOPO amewataka wananchi kutii sheria ya kilimo bora cha zao la pamba.

Mkuu wa mkoa wa TABORA amehitimisha ziara yake ya siku tano wilayani IGUNGA katika kampeni ya kuongeza tija katika kilimo cha zao la pamba ambapo wananchi pamoja na viongozi wa serikali ya vijiji na kata wamekula kiapo kusimamia vyema kilimo cha zao la pamba.

Asilimia 94 ya zao la pamba katika mkoa wa TABORA huzalishwa katika wilaya ya IGUNGA.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Rais Magufuli alifanyia mabadiliko baraza lake la mawaziri Tanzania.
Serikali imeshauriwa kuangalia upya sheria ya elimu namba 25 ya mwaka 1978 kuhusu adhabu ya kufutwa shule kwa mwanafunzi asiyehudhuria shuleni kwa muda wa siku 90 mfululizo ili kukabiliana na tatizo la utoro kwa wanafunzi.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise