Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Madereva wa vyombo vya moto nchini watashurutishwa endapo watavunja…

  • December 21, 2017

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini, kamishna msaidizi mwandamizi, FORTENATUS MUSILIMU amesema hayo wakati akizungumza na maderevya hao katika kituo cha MABASI cha zamani na kipya mkoani TABORA.

Amewataka madereva wote kutimiza vigezo vya usafiri kwanza ndipo wapeleke vyombo vyao barabarani, kinyume na hivyo watakamatwa na kufungiwa leseni zao.

Baadhi ya madereva wamempongeza kamanda MUSILIMU kwa mikakati yake ambapo pamoja na mambo mengine wameeleza uhusiano wao na Askari wa usalama barabarani mkoani TABORA kuwa sio mzuri.

Aidha kamanda MUSILIMU ameendesha zoezi la kukagua abiria katika mabasi na kupima madereva kama wanatumia kilevi katika kituo kipya cha mabasi.

Dereva aliyepimwa na kubainika hatumii kilevi anayeendesha gari kutoka USINGE hadi BARIADI OMARI KASIMU, amesema ili kutowachukia Askari wa usalama barabarani ni vema madereva kufuata sheria kama zilivyo.

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini,kamishna msaidizi mwandamizi, FORTENATUS MUSILIMU yupo katika ziara mkoani TABORA kukagua hali ya usalama barabarani na kuzungumza na madereva wa vyombo vya moto pamoja na abiria lengo ni kupunguza na kumaliza ajali barabarani.

 

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

TABORA: Jamii imetakiwa kuwa na utamaduni wa kuvaa vazi la suti.
Shirika la maendeleo ya jamii -CARITAS TABORA chini ya kanisa KATOLIKI limetoa mbegu za MIHOGO aina ya MKOMBOZI .

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise