Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Magufuli na Museveni waweka jiwe la msingi la bomba…

  • November 10, 2017
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli na Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda.

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli na Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda wameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa bomba kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania.

Rais hao wawili wameweka jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi wakiwa katika kijiji cha Luzinga, jirani na mpaka wa Mutukula.

Pia wamefungua kituo cha forodha chenye huduma zote muhimu kurahisisha safari kati ya nchi hizo mbili.

Rais Magufuli anafanya ziara Uganda kwa siku tatu.

Ujenzi wa mradi wa bomba la mafuta ghafi la Hoima -Tanga wenye urefu wa jumla ya Kilometa 1,443 zikiwemo 1,115 zitakazojengwa ndani ya ardhi ya Tanzania utagharimu dola za marekani bilioni 3.55, unatarajiwa kusafirisha mapipa laki 2 ya mafuta kwa siku na wakati wa ujenzi unatarajiwa kuzalisha ajira kati ya 6,000 na 10,000. Bomba linatarajia kukamilika mwaka 2020.

Mradi huo utakao gharimu dola za kimarekani bilioni 3 unajengwa kwa ushirikaino wa serikali za nchi hizo mbili na washirika na unatariji kutoa ajira zaidi ya 30,000.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

TABORA: Serikali inaendelea na juhudi ya kuhakikisha tumbaku inanunuliwa.
Ahukumiwa kifungo cha maisha kwa kubaka mwanafunzi.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Mazishi ya pacha Maria na…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise