Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Makubaliano kuhusu nyuklia ya Iran yana kasoro.

  • May 17, 2018

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema nchi za Umoja wa Ulaya zinakubali kwamba Makubaliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran yana mapungufu, lakini pia zimekubaliana kuwa yanapaswa kuendelezwa.

Viongozi wa nchi 28 za Umoja wa Ulaya wanaokutana katika mji mkuu wa Bulgaria Sofia, wameweka mshikamano katika kuyanusuru makubaliano hayo yaliyosainiwa mwaka 2015, baada ya Rais Donald Trump kuiondoa Marekani, na kurejesha vikwazo dhidi ya Iran, akilalamikia mpango wa makombora wa nchi hiyo na kujiingiza kwake katika mizozo ya Mashariki ya Kati.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron pia amesema Ulaya inafanya juhudi kuyaokoa makubaliano hayo, ili iweze kuendeleza biashara na Iran. Iran imetoa tahadhari kwamba inaweza kuanzisha urutubishaji wa madini ya Urani bila kikomo, ikiwa Ulaya itashindwa kuihakikishia kwamba faida zitokanazo na kuondolewa kwa vikwazo chini ya makubaliano hayo zitaendelea kupatikana.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Watanzania wataka elimu iboreshwe- Utafiti.
Watu walio na virusi vya Ebola Congo wameongezeka

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise