Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Marekani yawafukuza wanadiplomasia 15 wa Cuba.

  • October 4, 2017
Marekani yawafukuza wanadiplomasia 15 wa Cuba.

Marekani imewafukuza wanadiplomaisa 15 wa Cuba ikisema kwa Cuba ilistahii kuwalinda wanadiplomasia wa Marekani kutokana mashambulizi ya kutumia sauti.

Waziri wa mambo ya kigeni nchini Cuba Bruno Rodriguez ameitaja hatua hiyo ya Marekani kuwa isiyokubalika.

Hatua hiyo ya wizara ya mambo ya kigeni inafuatia hatua ya Marekani ya kuwaondoa zaidi ya nusu ya wanadiplomasia wake kutoka mji mkuu wa Cuba.

Karibu watu 20 raia wa Marekani wamepatwa na matatizo ya kiafya mjini humo.

Nao wanadiplomasia wa Cuba wamepewa muda wa siku saba kuondoka Marekani.

Takriban watu 21 wanaofanya kazi kwenye ubalozi wa Marekani nchini Cuba wamelalamikia matatizo ya kiafya yakiwemo kupoteza uwezo wa kusikia na kisungusungu.

Ripoti za awali zinasema kuwa mashambulizi ya kutumia sauti ndiyo yalichangia.

Cuba imekana kuwalenga wafanyakazi wa ubalozi wa Marekani na Marekani yenyewe haijailaumu serikali ya Cuba kwa mashambulizi hayo.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Catalonia kutangaza uhuru ‘siku chache zinazokuja’.
Mtu mmoja amekufa baada ya kugongwa na kiberenge katika mtaa wa MKONKOLE,kata ya TAMBUKARELI mjini TABORA.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Guardiola alinichukulia kama adui na…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise