Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Mtanzania akamatwa na dhahabu ya $1m Nairobi

  • February 22, 2018

Maafisa wa forodha nchini Kenya wamemkamata mwanamume anayedaiwa kuwa raia wa Tanzania katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta, Nairobi akisafirisha dhahabu ya thamani ya dola milioni moja, taarifa zinasema.

Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 46 anadaiwa kuwasili kutoka Mwanza, Tanzania kupitia uwanja wa Kilimanjaro na alikuwa safarini kuelekea Dubai.

Gazeti la kibinafsi ya Nation linasema mwanamume huyo, ambaye jina lake halijafichuliwa kufikia sasa, aliwasili uwanja wa JKIA Ijumaa 16 Februari akiabiri ndege ya Precisio Airlines na alitaka kuabiri ndege ya Kenya Airways kuelekea Dubai.

Maafisa wa uIdara ya Uchunguzi wa Jinai wakiandamana na maafisa wa uchunguzi kutoka Mamlaka ya Mapato ya Kenya (KRA) walimhoji na akaandikisha taarifa.

Kwa nini akakamatwa?

Sheria za Usimamizi wa Forodha za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) za mwaka 2004, kKifungu 85(3) na Kiambatisho cha Pili Sehemu B (4) huharamisha usafirishaji wa madini ambayo hayajapitia viwandani katika kanda ya Afrika Mashariki.

Vipande hivyo vya dhahabu vya uzani wa kilo 32.3 vinashikiliwa na maafisa wa idara ya forodha wa KRA huku uchunguzi zaidi ukiendelea.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Serikali inatarajia kuajiari walimu wa shule ya msingi na sekondari 11,000.
Sababu tano zinazozuia mageuzi kuhusu umiliki wa bunduki Marekani

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise