Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Mwanamke afutwa kazi kwa kuuonyesha msafara wa Trump kidole…

  • November 7, 2017
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 50 anasema kuwa hajuti kufutwa kazi.

Mwanamke aliyepigwa picha akiuonyesha msafara wa rais Donald Trump ishara ya kidole cha kati ameripotiwa kufutwa kazi na kampuni iliomuajiri kufutia picha hiyo.

Picha hiyo ilisambazwa baada ya kupigwa mnamo terehe 28 mwezi Oktoba mjini Virginia karibu na uwanja wa kucheza Gofu wa Trump.

Juli Briskman ambaye alitambulika kama mwendesha baiskeli anadai kwamba alifutwa kazi na mwajiri wake Akima LLC baada ya kuichapisha katika mtandao wake.

Kampuni hiyo hatahivyo haikutoa tamko lolote ilipotakiwa kufanya hivyo na BBC.

Bi Briskman aliambia vyombo vya habari kwamba kampuni hiyo ilimuita katika mkutano siku moja baada ya kumwambia afisa mkuu wa ajira kwamba ni yeye ndiye aliyepiga picha hiyo.

Alilimbia gazeti la Huffington Post kwamba maafisa wakuu wa kampuni hiyo walimwambia kwamba picha hiyo imeorodheshwa kama chafu na kwamba ilikiuka viwango vya sera za mitandao baada ya kuichapisha katika akaunti zake za Twitter na facebook.

Hatahivyo bi Briskman alisema kuwa aliusisitizia usimamizi wa kampuni hiyo kwamba hakuwa akifanya kazi wakati picha hiyo ilipopigwa na kwmaba hakuwataja waajiri wake katika mtandao huo wa kijamii.

Bi Briskman anasema kuwa mwenzake wa kiume hakufutwa kazi baada ya kufuta picha iliodaiwa kuwa chafu katika kisa chengine.

Hivyobasi amekuwa akihoji ni kwa nini alifutwa kazi mara moja.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 50 ambaye ana watoto wawili ameripotiwa kufanya kazi katika kampuni hiyo ya serikali kwa miezi sita akifanya kazi ya mawasiliano.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

TABORA: Wahitimu wa VETA watakiwa kutumia uuzi wao kujikwamua kiuchumi.
Kipimo cha pumzi kugundua Malaria chaonyesha matumaini

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise