Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Mwanamume achoma moto nyumba akiua buibui California, Marekani

  • January 11, 2018January 11, 2018

Mwanamume mmoja katika mji wa Redding kaskazini mwa California, Marekani anadaiwa kuchoma moto nyumba akijaribu kumuua buibui.

Kisa hicho kilitokea Jumapili kwa mujibu wa vyombo vya habari Marekani.

Mmoja wa walioshuhudia, ambaye alikuwa anaishi katika nyumba hiyo kubwa ya makazi, ameambia gazeti moja California kwamba buibui huyo huenda alichangia kueneza moto huo chumbani, akikimbia akiwa anaungua.

Haijabanika iwapo buibui huyo alinusurika.

Hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa, lakini wakazi wa jumba hilo waliondolewa.

Afisa wa idara ya wazimamoto eneo hilo Gerry Gray ameambia BBC ni kwenye kwamba moto ulizuka katika jumba hilo lakini akasema chanzo cha moto huo bado kinachunguzwa.

“Taarifa kuhusu ‘buibui’ zilitolewa na raia walioshuhudia, waliokuwa eneo la mkasa, na bila shaka zinatumiwa katika uchunguzi.

Buibui huyo alikuwa aina ya ‘wolf spider’ ambao ni buibui wakubwa.

Idara ya kuzima moto imeambia gazeti la Redding Record Searchlight kwamba dalili zinaonesha moto huo uliwashwa kwa mwenye.

Redding, eneo ambalo kisa hicho kilitokea, ni mji ulio maili 162 (261km) kaskazini Sacramento.

Walioshuhudia wanasema buibui huyo alieneza moto alipokimbia na kujificha kwenye mto.

Mto huo ulishika moto na moto huo, na ingawa wakazi waliweza kuuzima hapo, ulikuwa tayari umeenea maeneo mengine ya jumba hilo.

Maafisa wanasema moto huo ulisababisha uharibifu wa takriban $11,000 (£8,000) na baadhi ya vyumba vya jumba hilo vitahitaji kukarabatiwa kabla ya watu kuishi huko tena.

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Meli yenye bendera ya Tanzania yanaswa Ugiriki ikipeleka vilipuzi Libya
Mkuu wa genge la Yakuza la Japan akamatwa Thailand

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise