Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Rais Daktari JOHN MAGUFULI amewasisitiza watanzania kuendelea kulipa kodi…

  • March 14, 2018

Rais Daktari JOHN POMBE MAGUFULI amewasisitiza watanzania kuendelea kulipa kodi ili kuwezesha miradi mbali mbali kutekelezwa ukiwemo mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa-Standard Gauge.

Akizungumza katika stesheni ya IHUMWA wakati wa uzinduzi na uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa reli ya kisasa awamu ya pili kutoka MOROGORO hadi MAKUTUPORA mkoani DODOMA,Rais MAGUFULI amesema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kuajiri Watanzania wengi.

Awali akitoa salamu za mkoa,mkuu wa mkoa wa DODOMA, BINILITH MAHENGE amesema wameanza kuwaandaa vijana ili wanufaike na ujenzi wa reli ya kisasa na kwamba wananchi wa DODOMA hawatamwangusha Rais MAGUFULI.

Kwa upande wake,Balozi wa UTURUKI,ALI GAITOL amesema ujenzi wa reli ya kisasa siyo tu utarahisisha usafirishaji,lakini pia utachochea maendeleo ya nchi na utasaidia kuimarisha mahusiano kati ya serikali ya UTURUKI na TANZANIA katika maeneo mbalimbali.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli TANZANIA-TRC-, MASANJA KADOGOSA amesema kutokana na kasi ya ujenzi wa reli hiyo,baadhi ya wananchi watafuatwa na kulipwa fidia ili kupisha ujenzi wa reli.

Mbunge wa DODOMA Mjini,ANTONY MAVUNDE ameipongeza serikali ya Awamu ya Tano akisema kuwa ni sikivu kwa sababu imesaidia jimbo lake kupata huduma ya maji huku akiahidiwa kupata umeme mkoa mzima.

Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi,Profesa MAKAME MBARAWA amesema hadi sasa awamu ya kwanza ya mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa umeajiri Watanzania 2,100 ambayo ni fursa kwa wananchi.

Ujenzi wa mradi wa reli ya kisasa-STANDARD GAUGE ulianza rasmi Februari 26 mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Februari 25 mwaka 2021.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Mwanafizikia Stephen Hawking afariki dunia
TABORA: Jeshi la polishi kuwashughulikia askari polisi wanaopokea rushwa.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise