Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Rais MAGUFULI amewaagiza mabalozi wa TANZANIA kutafuta masoko ya…

  • June 4, 2018

Rais JOHN MAGUFULI amewataka mabalozi wanaoiwakilisha TANZANIA katika nchi mbalimbali duniani kuhakikisha wanatafuta masoko ya bidhaa za kilimo.

Rais MAGUFULI ametoa agizo hilo wakati wa uzinduzi wa programu ya kuendeleza  sekta ya kilimo awamu ya pili katika ukumbi wa Mwalimu NYERERE jijini DAR ES SALAAM akisema  uzalisahaji wa mazao utakapoongezeka ni lazima mabalozi wahakikishe TANZANIA  inakuwa na soko la uhakika la kuuzia mazao ya bidhaa za kilimo.

Kwa upande wake,Mratibu wa Programu ya Kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili,Mhandisi JANUARY KAYUMBE amesema lengo la utekelezaji wa programu hiyo  kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo, kubadilisha mfumo wa kilimo wa uendeshaji wa shughuli za kilimo kuwa za kibiashara  na baadaye kukuza uchumi wa nchi.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima,wafugaji ,wavuvi na wafanyabiashara MAGEMBE MAKOYE amesema wako tayari kushirikiana na wataalamu na viongozi kuhakikisha wanafikia lengo lililokusudiwa na kuiomba serikali kuimarisha upatikanaji wa pembejeo za kilimo.

Naye Mwenyekiti wa Sekta Binafsi,Dakta REGINALD MENGI amesema sekta hiyo inaunga mkono programuu hiyo yenye lengo la kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo na kupandisha kipato cha mkulima.

Rais MAGUFULI pia ameitaka Benki ya Kilimo TANZANIA kuacha kuwakopesha matajiri badala yake iwakopeshe wakulima wadogo wadogo kwa sababu benki hiyo imeanzishwa kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.

MWANDISHI: STEPHANIA LAISON,CGFM

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Pellegrini aporwa na majambazi wenye bunduki
ISRAEL: Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu anaanza ziara barani Ulaya.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise