Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
HAKI MILIKI Yetu Media Local

RAIS MAGUFULI: Mfumo wa utoaji wa haki nchini bado…

  • February 1, 2018

Mwandishi: Najjat Omar

Rais JOHN POMBE MAGUFULI amesema usimamizi wa sheria na mfumo wa utoaji wa haki nchini bado unakabiliwa na matatizo mengi ikiwemo kupungua kwa maadili kwa watumishi wachache wenye dhamana ya kusimamia sheria. 

Rais MAGUFULI ametoa kauli hiyo wakati wa akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini akisema kuwa watumishi hao wachache hawapaswi kuachwa.

Rais MAGUFULI amesema hakuna mtu anayependwa kufukuzwa kazi,lakini Jaji Mkuu,Profesa IBRAHIM JUMA IBRAHIMa mefanya jambo jema kuwastaafisha watumishi hao.

Rais pia amevitaka vyombo ya usalama nchini kuiga mfano wa Jaji Mkuu kwa kuhakikisha wanatimia wajibu wao.

Kwa upande wake,Jaji mkuu wa TANZANIA,Profesa IBRAHIM JUMA amesema hataki kusikia kuwa jalada la kesi halionekani,limepotea wala kucheleweshwa kwa kesi.

Pia amewataka ,Majaji ,mahakimu na Watendaji wa mahakama kubadilika na kuendana na mabadiliko ya  Teknolojia,Habari na Mawasiliano –TEHAMA kwa sababu mahakama zote nchini zitaungwanishwa katika mtandao wa TEHAMA.

Naye Makamu wa Rais wa Chama cha Mawakili TANGANYIKA,GODWIN GWIMILINI amesema kuwa lazima kuwepo na usawa wa mahitaji ya huduma na matakwa ya utawala.

Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini mwaka yanaambatana na Kauli mbiu ya  “Matumizi ya TEHAMA katika utoaji Haki kwa wakati na kuzingatia maadili.”

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Diwani wa kata ya KABILA ajiuzulu na kujiunga na CCM
TABORA: TAKUKURU yawaonya wanaotishia usalama wa wanawaripoti wala rushwa.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise