Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa Kusimamia kombe la dunia…

  • June 7, 2018

Takriban maafisa 100 wa kandanda katika eneo la Afrika Magharibi na Kenya walipatikana katika kamera wakipokea fedha katika operesheni kali.

Ni miongoni mwa upelelezi wa miaka miwili uliofanywa na mwandishi wa Ghana mwenye utata Anas Aremeyaw Anas.

Katika kisa kimoja naibu refa kutoka Kenya anayeelekea Urusi kuchezesha dimba la dunia kutoka Kenya alikubali dola 600 kutoka kwa mtu aliyejifanya kuwa afisa wa shirikisho la soka la Ghana.

Fifa inasema kuwa refa huyo kwa Jina Aden Range Marwa , ambaye ni mmojawapo wa marefa walioteuliwa na Fifa kushiriki katika kombe la dunia nchini Urusi , hataelekea tena Urusi baada ya kupatikana akipokea zawadi ya $600.

Marwa alipewa fedha hizo na mwandishi mpelelezi aliyejifanya kuwa afisa mkuu wa timu moja kuu ya Ghana. Hatahivyo refa huyo amekana kufanya makosa yoyote.

Mwanachama wa baraza la Fifa nchini Ghana Kwesi Nyantakyi , ambaye ndiye afisa wa pili kwa uwezo katika soka ya Afrika , pia alipatikana na operesheni hiyo kali.

Alionekana akipokea $65,000 kutoka kwa mwandishi mpelelezi aliyejifanya kuwa mwekezaji katika soka ya Ghana.

Nyantakyi amekataa kutoa tamko lolote. Kwa jumla zaidi ya marefa 100 na maafisa wakuu walipatikana katika kamera wakichukua fedha kinyume na sheria za Fifa na GFA .

Makala hiyo iliofanywa na mwandishi aliyezua utata Anas Aremayaw Anas imezua maswali makali kuhusu hatma ya mchezo wa kandanda wenye ushabiki mkubwa barani Afrika.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Mazishi ya pacha Maria na Consolata Tanzania
Msanii Sam wa Ukweli ameaga Dunia.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…
Burundi kuitambulisha katiba mpya siku…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise