Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Seneti Marekani laidhinisha matumizi ya shughuli za serikali

  • January 23, 2018

Bunge la Seneti nchini Marekani limeidhinisha matumizi ya muda kufadhili shughuli za serikali katika kumaliza mjadala uliozua sitofahamu kwa siku tatu.

Muswada huo, ulioidhinishwa na idadi kubwa ya maseneta, utasaidia kufadhili huduma za serikali kwa wiki nyingine mbili na nusu.

Muswada huo pia umepelekwa baraza la wawakilishi na baadaye kusainiwa na Rais Trump.

Wawakilishi wa chama cha Democratic walisema kuwa wataunga mkono muswada huo kama utatoa hatma ya maelfu ya wahamiaji waliongia marekani wakiwa watoto ambapo sasa wanakabiliwa na kurudishwa sehemu walizotoka.

Hadi sasa wahamiaji hao wanalindwa na mpango wa kuwasadia watu walioingia Marekani wakiwa watoto DACA.

Akizungumza baada ya kura hizo za seneti, kiongozi wa chama cha Republic Mitch McConnell amezitaka pande zote mbili kufikia makubaliano yenye tija.

Chanzo: BBC Swahili

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Wanawake kuandamana kuhusu madai ya ubakaji katika hospitali Kenya.
Kamati ya Ushauri ya Manispaa ya TABORA imepitisha mapendekezo ya rasimu ya mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2018-2019.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise