Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Serikali imeshauriwa kutekeleza sheria kwa watu wanaofanya vitendo vya…

  • December 7, 2017

Serikali imeshauriwa kutekeleza sheria kwa watu wanaofanya vitendo vya ukatili ili kutokomeza tatizo hilo katika jamii. Wito huo umetolewa na ROSEMARY SILILI wakati wa zoezi la kalamu na ubao linaloendeshwa na CGFM katika kata ya MAPAMBANO,eneo la SOKONI ikiwa ni sehemu ya kampeini yake ya kupinga ukatili wa kijinsia.

Amesema endapo elimu itatolewa kwa watu sambamba na utoaji wa adhabu kali kwa watu wanaofanya vitendo vya ukatili basi wengi wao wataogopa kujihusisha na vitendo hivyo.

Kwa upande wake RASHIDI MAKULA amewashauri vijana wa jinsia zote kuzingatia  maadili hasa katika kuvaa mavazi ya heshima ili kuwa mfano wa kuigwa katika jamii.

Naye PRISCA RICHARD amemuunga mkono akisema wanawake  wanaovaa  mavazi yasiyo ya maadili yanawadhalilisha katika jamii inayowazunguka.

Hali kadhalika,JOHARI HASSAN amesema vitendo vingine vya ukatili wa kujinsia wanavyofanyiwa wanawake ni kutokana na wanaume kutelekeza familia zao kwa kigezo cha kuwa na maisha magumu.

Akizungumzia malalamiko ya wanaume kuwatelekeza wanawake, RASHIDI MAKULA amesema wanaume hufanya hivyo kutokana na manyanyaso wanayofanyiwa na wenza wao.

Wanawake na watoto mkoani TABORA ni makundi ambayo hufanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kiasi kikubwa kama ubakwaji na kulawitiwa jambo ambalo limetakiwa kupingwa na wananchi kwa nguvu zote.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Liverpool, Monaco, Spurs zamaliza hatua ya makundi kwa ushindi.
Taasisi za Uma na Binafsi zimehimizwa kutoa kipaumbele kwa vijana wanaojitolea maofisini hasa zinapotokea fursa za ajira.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise