Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Serikali imetenga fedha kwa ajili ya Mfuko wa Watu…

  • June 5, 2018

Serikali imetenga fedha kwa ajili ya Mfuko wa Watu wenye Ulemavu katika mwaka ujao wa fedha 2018-2019.

Kauli hiyo imetolewa bungeni jijini DODOMA na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu –Sera,Bunge,Ajira na Watu wenye ulemavu,STELLA IKUPA wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum AMINA MOLELI  aliyetaka kujua ni lini serikali itatenga fedha kwa ajili ya mfuko wa watu wenye ulemavu.

Akiuliza maswali mawili ya nyongeza mbunge wa viti maalum AMINA MOLELI amehoji ni lini serikali itaunda Baraza la Watu wenye Ulemavu.

Akijibu maswali hayo,Naibu Waziri STELLA IKUPA amekiri kuwa muda wa wajumbe wa baraza la watu wenye walemavu kuongoza baraza hilo umekwisha.

Baraza la watu wenye ulemavu lilianzishwa kwa mujibu wa lengo la kuwezesha utekelezaji wa majukumu ya Baraza la Taifa la Ushauri kwa watu wenye ulemavu, hivyo serikali inajipanga kuhakikisha wanapatikana watu waaminifu na wenye uwezo wa kuwasilisha matatizo ya watu wenye ulemavu kwa muda muafaka.

MWANDISHI: ANGEL MTAKI,CGFM

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Serikali kuwalipa fidia wananchi wa Igunga waliopitiwa na bomba la mafuta la Hoima.
Mashabiki wa klabu ya YANGA wilayani KALIUA wanaamini timu yao itarejea katika hali ya kawaida uwanjani

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali kuwalipa fidia wananchi wa…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise