Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Serikali kuendelea kuratibu mpango wa kutoa chaakula Shuleni.

  • May 10, 2018

Serikali imesema inaendelea kuratibu mpango utakaowawezesha kuanza kutoa chakula shuleni kwa wanafunzi wa shule za sekondari za kutwa na shule za msingi ili wanafunzi waweze kusoma vizuri.

Waziri Mkuu,KASSIM MAJALIWA ameeleza hayo bungeni jijini DODOMA wakati akijibu maswali ya papo kwa papo ambapo amesema suala la chakula ni muhimu kwa wanafunzi lakini serikali haiwezi kutoa chakula kwa shule zote zilizopo nchini.

Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa TEMEKE,ABDALA MTOLEA ambaye alitaka kujua ni lini serikali itabadilisha sera ya elimu bure ili chakula shuleni liwe suala la lazima.

Waziri Mkuu amesema mpango wa elimu bure unaratibiwa kadri ya mahitaji na kuwa suala la chakula kwa sasa wazazi wanaweza kuona umuhimu wa kupeleka chakula shuleni.

Waziri Mkuu amewasihi wazazi kuendelea kushirikiana na serikali pamoja na wadau katika kuimarisha elimu na kutafuta njia bora ya kuboresha elimu ikiwemo utoaji wa huduma bora kwa watoto ili waweze kusoma vizuri na kwamba siyo  lazima chakula kiwe wali au ugali hata uji unatosha.

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Malaysia yapata kiongozi mkongwe zaidi duniani aliyechaguliwa
Serikali yakanusha tuhuma za kukandamiza haki za Wamaasai

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise