Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
News

Serikali ya Nigeria yaongeza nguvu kuwasaka wasichana waliotekwa.

  • February 26, 2018February 26, 2018

Mamlaka nchini Nigeria imesema imeongeza nguvu ya ndege za kivita ili kuweza kuwasaka wanafunzi wasichana waliotekwa Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.

Serikali inasema takriban wasichana 110 hawajulikani walipo baada ya wanamgambo wa kiislam kuwateka katika shule yao iliyopo Dapchi.

Mapema serikali ya kijiji hicho ilililaumu jeshi kwa kushindwa kuchukua hatua hata baada ya kupewa taarifa.

Rais Muhammadu Buhari ameelezea tukio hilo kama janga la taifa.

Hasira zimekuwa zikiwapanda wazazi wa wasichana hao huku kukiwa na ripoti kuwa wanajeshi walikuwa wameondolewa kutoka kwa vizuizi vikuu vya Dapchi mwezi uliopita.

Dampchi ambao ni mji ulio kilomita 275 kaskazini magharibi wa Chibok, ulishambuliwa siku ya Jumatatu, na kusababisha wanafunzi na walimu kutoka shule moja ya serikali kukimbiliaa vichakani.

Wenyeji wanasema vikosi vya jeshi la Nigeria vikisaidiw na ndege za vita baadaye vilizima uvamizi huo.

Mamlaka awali zilikana kuwa wasichana hao walikuwa wametekwa, zikisema kuwa walikuw wamejificha kutoka kwa wanamgambo hao.

Lakini baadaye wakakiri kuwa wasichana 110 walikuwa hawajulikani waliko baada ya uvamizi huo.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Sababu tano zinazozuia mageuzi kuhusu umiliki wa bunduki Marekani
Wanawake 15 wapiganaji wa IS raia wa Uturuki wahukumiwa kifo Iraq

Related articles

Guardiola alinichukulia kama adui na…
TABORA: Ushiriki wa wazazi kusoma…
Milioni 334 zatengwa kwa ajili…
Macron aanza ziara yake nchini…
Mwakyembe aagiza Nandy akamatwe, Diamond…
Arsenal yanusurika kombe la Yuropa,…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise